Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko RITA kuwafuata wananchi mikoani
Habari Mchanganyiko

RITA kuwafuata wananchi mikoani

Emmy Hudson, Kaimu Msajili Mkuu wa Vizazi na Vifo
Spread the love

WAKALA wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) umeanza maboresho ya Mkakati wa Usajili wa Matukio Muhimu ya Binadamu na Takwimu (CRVS) ambao utatatua changamoto  zinazosababisha wananchi wengi kushindwa kujisajili kutokana na sababu mbalimbali, anaandika Jovina Patrick.

Emmy Hudson, Kaimu Msajili Mkuu wa Vizazi na Vifo amesema kuwa mkakati wa usajili umeanza kutekelezwa  kwa kundi la watoto  wenye umri chini ya miaka mitano katika mikoa saba ambayo ni Mbeya, Mwanza, Iringa, Njombe, Geita, Songwe na Shinyanga.

“Mikoa hiyo watoto walio na umri chini ya miaka mitano watafanyiwa usajili na kupata vyeti vya kuzaliwa vinavyojazwa kwa mkono bila kutozwa malipo yoyote katika ofisi za watendaji wa kata na vituo vya huduma ya afya.

“Cheti cha kuzaliwa kilichojazwa kwa mkono ni cheti halali kama ilivyo kwa vilivyochapishwa kwa mashine hivyo vinaweza kutumika mahali popote kupata huduma,” anasema Emmy.

Mtendaji huyo amezitaka taasisi zote nchini kuvikubali vyeti hivyo vinapowasilishwa ili kupata huduma mbalimbali  na endapo kutakuwa na mashaka yoyote zisisite kuwasiliana na ofisi za RITA na sio kuvikataa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

RPC Dodoma akabidhiwa bunduki mbili za wahalifu

Spread the love  Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa ya Kulevya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yazindua huduma maalum kwa wastaafu

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua huduma maalum kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yazindua akaunti ya Kikundi

Spread the loveBenki ya NMB imezindua akaunti ya kikundi yenye  maboresho makubwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyakazi waidai STAMICO mishahara ya bilioni 1

Spread the loveWALIOKUWA wafanyakazi wa mgodi wa Shirika la Madini la Taifa...

error: Content is protected !!