Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Sirro abadilisha makamanda wa polisi
Habari Mchanganyiko

Sirro abadilisha makamanda wa polisi

Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Susan Kaganda, aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni
Spread the love

MKUU wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Simon Sirro, amefanya mabadiliko ya makamanda wa polisi katika maeneo kadhaa, anaandika Catherine Kayombo.

Miongoni mwa waliobadilishwa vituo vya kazi ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Susan Kaganda, aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, ambaye amepelekwa kuwa Mkuu wa Kitengo cha Mafao na Fidia, makao makuu ya polisi.

Nafasi ya Kaganda imechukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Murilo Jumanne Murilo, aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga.

Aliyeteuliwa kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ni Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Simon Haule, aliyekuwa afisa mnadhimu wa Polisi Mkoa wa Mara.

Kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi la Polisi kwa vyombo vya habari, iliyosainiwa leo na Msemaji wa Polisi, Barnabas Mwakalukwa, mabadiliko hayo ni ya kawaida ndani ya jeshi hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyakazi waidai STAMICO mishahara ya bilioni 1

Spread the loveWALIOKUWA wafanyakazi wa mgodi wa Shirika la Madini la Taifa...

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

Habari Mchanganyiko

Mfanyakazi CRDB atoa sababu za kubambikiwa kesi, hukumu Mei 30

Spread the love  MFANYAKAZI wa Benki ya CRDB, Ibrahim Masahi (40) ameieleza...

Habari Mchanganyiko

Waziri Ummy atangaza Tanzania kuwa kitovu cha utalii tiba

Spread the loveSERIKALI imesema imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha matibabu ya...

error: Content is protected !!