Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwambe kumrithi Kairuki TIC
Habari Mchanganyiko

Mwambe kumrithi Kairuki TIC

Spread the love

JOHN Magufuli, Rais wa Tanzania leo amefanya uteuzi mpya Geoffrey Idelphonce Mwambe kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC), anaandika Hamisi Mguta.

Awali nafasi hiyo ilikuwa chini ya Juliet Kairuki ambaye alitenguliwa na Rais Magufuli Aprili 24, mwaka huu baada kupatikana kwa taarifa kuwa tangu alipoajiliwa mwaka 2013 kiongozi huyo alikuwa hachukui mshahara wa serikalini.

Kabla ya uteuzi huo Mwambe alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Manyoni mkoani Singida ambapo anatakayechukua nafasi hiyo atatajwa baadaye.

Katika hatua nyingine Rais amemteua Clifford Tandari aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezazji Tanzania kuwa Katibu Tawala wa mkoa wa Morogoro nafasi ambayo ilikuwa chini ya John Ndunguru ambaye amestaafu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA wawanoa mama lishe 50 kukabiliana na majanga ya moto

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) kwa kushirikiana na...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!