Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Mwambe kumrithi Kairuki TIC
Habari Mchanganyiko

Mwambe kumrithi Kairuki TIC

Spread the love

JOHN Magufuli, Rais wa Tanzania leo amefanya uteuzi mpya Geoffrey Idelphonce Mwambe kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC), anaandika Hamisi Mguta.

Awali nafasi hiyo ilikuwa chini ya Juliet Kairuki ambaye alitenguliwa na Rais Magufuli Aprili 24, mwaka huu baada kupatikana kwa taarifa kuwa tangu alipoajiliwa mwaka 2013 kiongozi huyo alikuwa hachukui mshahara wa serikalini.

Kabla ya uteuzi huo Mwambe alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Manyoni mkoani Singida ambapo anatakayechukua nafasi hiyo atatajwa baadaye.

Katika hatua nyingine Rais amemteua Clifford Tandari aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezazji Tanzania kuwa Katibu Tawala wa mkoa wa Morogoro nafasi ambayo ilikuwa chini ya John Ndunguru ambaye amestaafu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

Habari Mchanganyiko

Uholanzi wampongeza Rais Samia kuimarisha vyombo vya habari, demokrasia

Spread the love  UBALOZI wa Uholanzi nchini Tanzania, umempongeza Rais Samia Suluhu...

error: Content is protected !!