Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Magufuli, Zitto, Mwigulu wanena kuhusu wanawake
Habari Mchanganyiko

Magufuli, Zitto, Mwigulu wanena kuhusu wanawake

Dk. John Pombe Magufuli, Rais wa Tanzania
Spread the love

VIONGOZI mbalimbali wa kisiasa pamoja na watu mashuhuri hapa nchini akiwemo Rais John Magufuli, wametoa salamu za kuwatakiwa heri wanawake katika kilele cha maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani, anaandika Pendo Omary.

Itakumbukwa kuwa maadhimisho ya kiserikali ya siku ya wanawake duniani, yanayofanyika hapa nchini yamebeba kauli mbiu inayosema, “Tanzania ya wiwanda: Wanawake ni msingi wa mabadiliko ya kiuchumi.”

Kauli za baadhi ya viongozi kuhusu siku hii;

Rais John Magufuli

“Nachukua nafasi hii kuwapongeza wanawake wote katika kusherehekea siku ya wanawake duniani. Aidha ninawapongeza wanawake wa Tanzania kwa kuendelea kuunga mkono juhudi za serikali katika maendeleo. Mungu awabariki wanawake wote.”

Ummy Mwalimu- Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

“Tuwekeze kwenye Elimu ya Wasichana. Hii ndiyo njia bora ya kuhakikisha wanawake wanashiriki kikamilifu kwenye ujenzi wa Tanzania ya viwanda. wekeza kwenye elimu ya msichana. Inalipa!”

Zitto Kabwe, Mbunge wa Kigoma Mjini

“Nimeshiriki siku ya wanawake duniani kwa kuandikisha kwenye Hifadhi ya Jamii (NSSF), vikundi vya wanawake wa kata za Buzebazeba na Machinjioni, Manispaa ya Kigoma Ujiji. Kwa mwaka huu wa fedha 2016/17 jumla ya wanawake 210 kutoka kata 7 wataandikishwa kwenye hifadhi ya Jamii kupitia mfuko wa NSSF.

“Kupitia mfuko wa Maendeleo ya Jimbo (CDCF) wanawake hawa watachangia asilimia 50 tu ya michango inayotakiwa, na asilimia 50 nyengine itachangiwa na mfuko wa maendeleo ya jimbo.”

Mwigulu Nchemba- Waziri wa Mambo ya Ndani

“Heri ya siku ya wanawake, mwanamke ni nembo ya familia. Utu, ujasiri, bidii, uaminifu na umoja. Najivunia uwepo wenu.”

Edda Sanga – Mkurugenzi Mtendaji Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA).

“Tulikotoka ni mbali na hakika tumepiga hatua kubwa, wanawake wameanza kuonekana kwenye kila sekta ikilinganishwa na wakati harakati hizi zinaanza.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wami Ruvu hawana deni la Rais Samia katika kutunza vyanzo vya maji

Spread the love  BODI ya Maji Bonde la Wami Ruvu, imeendelea kuchua...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari Mchanganyiko

Dk. Jafo aipongeza Oryx kumuunga mkono Samia

Spread the loveWAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

error: Content is protected !!