Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wema afikishwa mahakamani, aachiwa kwa dhamana
Habari MchanganyikoMichezo

Wema afikishwa mahakamani, aachiwa kwa dhamana

Wema Sepetu akiwasili kituo cha Polisi cha Kati
Spread the love

WEMA Sepetu na wenzake wawili wamefikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo na kusomewa mashitaka matatu yanayohusiana na matumizi ya dawa za kulevya aina ya bangi, anaaandika Mwandishi Wetu.

Akisomewa mashtaka na wakili wa serikali Nassoro Katuga mbele ya Hakimu Mkazi Thomas Simba imeelezwa kuwa msanii huyo alikutwa na kiwango kidogo cha dawa za kulevya aina ya bangi.

Wakili Nassoro Katuga amesema mahakamani hapo kuwa mtuhumiwa Wema Sepetu mnamo Februari 4, 2017 katika eneo la Kunduchi Ununio watuhumiwa watatu akiwemo Wema walitenda kosa hilo kinyume na kifungu cha sheria ya kuzuia na kupambana na dawa za kulevya kifungu cha 17 (1) (a) cha makosa hayo.

Msanii huyo na wenzake wameachiwa kwa dhamana ya Sh. milioni tano na wadhamini wawili na kesi hiyo imeahirishwa hadi Februari 22, 2017 itakapotajwa tena na kwamba bado uchunguzi unaendelea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

RPC Dodoma akabidhiwa bunduki mbili za wahalifu

Spread the love  Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa ya Kulevya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yazindua huduma maalum kwa wastaafu

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua huduma maalum kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yazindua akaunti ya Kikundi

Spread the loveBenki ya NMB imezindua akaunti ya kikundi yenye  maboresho makubwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyakazi waidai STAMICO mishahara ya bilioni 1

Spread the loveWALIOKUWA wafanyakazi wa mgodi wa Shirika la Madini la Taifa...

error: Content is protected !!