Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wema afikishwa mahakamani, aachiwa kwa dhamana
Habari MchanganyikoMichezo

Wema afikishwa mahakamani, aachiwa kwa dhamana

Wema Sepetu akiwasili kituo cha Polisi cha Kati
Spread the love

WEMA Sepetu na wenzake wawili wamefikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo na kusomewa mashitaka matatu yanayohusiana na matumizi ya dawa za kulevya aina ya bangi, anaaandika Mwandishi Wetu.

Akisomewa mashtaka na wakili wa serikali Nassoro Katuga mbele ya Hakimu Mkazi Thomas Simba imeelezwa kuwa msanii huyo alikutwa na kiwango kidogo cha dawa za kulevya aina ya bangi.

Wakili Nassoro Katuga amesema mahakamani hapo kuwa mtuhumiwa Wema Sepetu mnamo Februari 4, 2017 katika eneo la Kunduchi Ununio watuhumiwa watatu akiwemo Wema walitenda kosa hilo kinyume na kifungu cha sheria ya kuzuia na kupambana na dawa za kulevya kifungu cha 17 (1) (a) cha makosa hayo.

Msanii huyo na wenzake wameachiwa kwa dhamana ya Sh. milioni tano na wadhamini wawili na kesi hiyo imeahirishwa hadi Februari 22, 2017 itakapotajwa tena na kwamba bado uchunguzi unaendelea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!