Monday , 5 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea kurudi tena Ubungo
Habari za SiasaTangulizi

Kubenea kurudi tena Ubungo

Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo (mwenye miwani) akiwa katika moja ya ziara zake katika jimbo lake
Spread the love

MBUNGE wa Ubungo (Chadema), Saed Kubenea, ataendelea na ziara yake ya kikazi – kiserikali – ndani ya jimbo lake, kuanzia Jumatatu ya tarehe 6 Machi hadi tarehe 12 Machi 2017, anaandika Bupe Mwakiteleko.

Katika ziara hiyo, Kubenea atatembelea kata za Ubungo, Sinza, Kimara na Mburahati kwa lengo la kukagua shughuli za kiserikali kwa maana ya miradi ya maendeleo; kukutana na wananchi na kusikiliza kero zao; kuwafafanulia mambo mbalimbali yanayowahusu na baadaye kuhutubia mikutano ya hadhara.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na ofisi ya mbunge huyo, tarehe 6 Machi 2017, Kubenea atakuwa Kata ya Ubungo, tarehe 8 Machi (Jumatano), atakuwa kata ya Sinza, tarehe 10 Machi (Ijumaa), atakuwa Kata ya Kimara na tarehe 12 Machi (Jumapili), atakuwa Kata ya Mburahati.

“Hii ni awamu ya pili ya ziara ya Kubenea katika jimbo lake. Tayari ameshatembelea kata za Mabibo, Makuburi na Makurumla, ambako alikutana na wananchi na alihutubia mkutano wa hadhara,” imeeleza taarifa ya mbunge kwa wananchi.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, ziara za mbunge huyo, zinatarajiwa kuanza kuanzia saa 5 asubuhi na kukamilika saa 10 jioni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

MichezoTangulizi

Yanga malizeni ugomvi na Fei Toto – Rais Samia

Spread the love  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kifo cha mwanafunzi UDOM: Tume yamsafisha naibu waziri

Spread the loveTUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini (THBUB),...

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

error: Content is protected !!