Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea kurudi tena Ubungo
Habari za SiasaTangulizi

Kubenea kurudi tena Ubungo

Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo (mwenye miwani) akiwa katika moja ya ziara zake katika jimbo lake
Spread the love

MBUNGE wa Ubungo (Chadema), Saed Kubenea, ataendelea na ziara yake ya kikazi – kiserikali – ndani ya jimbo lake, kuanzia Jumatatu ya tarehe 6 Machi hadi tarehe 12 Machi 2017, anaandika Bupe Mwakiteleko.

Katika ziara hiyo, Kubenea atatembelea kata za Ubungo, Sinza, Kimara na Mburahati kwa lengo la kukagua shughuli za kiserikali kwa maana ya miradi ya maendeleo; kukutana na wananchi na kusikiliza kero zao; kuwafafanulia mambo mbalimbali yanayowahusu na baadaye kuhutubia mikutano ya hadhara.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na ofisi ya mbunge huyo, tarehe 6 Machi 2017, Kubenea atakuwa Kata ya Ubungo, tarehe 8 Machi (Jumatano), atakuwa kata ya Sinza, tarehe 10 Machi (Ijumaa), atakuwa Kata ya Kimara na tarehe 12 Machi (Jumapili), atakuwa Kata ya Mburahati.

“Hii ni awamu ya pili ya ziara ya Kubenea katika jimbo lake. Tayari ameshatembelea kata za Mabibo, Makuburi na Makurumla, ambako alikutana na wananchi na alihutubia mkutano wa hadhara,” imeeleza taarifa ya mbunge kwa wananchi.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, ziara za mbunge huyo, zinatarajiwa kuanza kuanzia saa 5 asubuhi na kukamilika saa 10 jioni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!