Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Watatu wapoteza maisha ajali ya ndege Bukoba
Habari MchanganyikoTangulizi

Watatu wapoteza maisha ajali ya ndege Bukoba

Spread the love

WATU watatu kati ya 27 waliookolewa hadi sasa wameripotiwa kupoteza maisha katika ajali ya ndege ya Kampuni ya Precision iliyotokea Bukoba mkoani Kagera. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Vifo hivyo vimethibitishwa na taarifa ya Msemaji wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji makao makuu Dodoma, P. E. Nzalayaimisi.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa jeshi hilo linaendelea na juhudi za kuokoa abiria wengine 16 waliobaki ndani ya ndege na kuwataka Watanzania kuendelea kuwa watulivu.

https://youtu.be/2EwivzgaJzs

Mkuu wa Mkoa wa Kagera amesema Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa anatarajia kuwasili eneo la tukio muda wowote kuanzia sasa.

Ndege ya Precision yenye mruko namba PW 494 ikitokea Dar es Salaam kwenda Kagera ikiwa na abiria 39 akiwemo mtoto mchanga, ilipata ajali na kutua ndani ya Ziwa Victoria umbali mdogo kutoka uwanja wa ndege wa Bukoba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!