Wednesday , 1 May 2024
Home Habari Mchanganyiko 13 wafariki dunia ajali ya basi likigonga treni Singida
Habari MchanganyikoTangulizi

13 wafariki dunia ajali ya basi likigonga treni Singida

Spread the love

JUMLA ya watu 13 wakiwamo wanawake sita na wanaume saba wamefariki dunia baada ya basi la kampuni ya Ally’s Star Bus kugonga kichwa cha treni chenye namba V951 90O06 kilichokuwa kikitokea Stesheni ya Aghondi kuelekea Manyoni katika makutano ya reli na barabara eneo la Manyoni mkoani Singida.

Basi hilo la abiria lenye namba za usajili T178 DVB mali ya kampuni ya Ally’s Star Bus limepata ajali alfajiri ya leo tarehe 29 Novemba 2023. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano kutoka Shirika la Reli Tanzania (TRC), Jamila Mbarouk imesema ajali hiyo imesababisha pia majeruhi 25.

“Ajall imehusisha basi la abiria lililokuwa likivuka njia ya reli eneo la Kilomita 587 Manyoni na kichwa cha treni na kusababisha majeruhi 25 kati yao wanawake saba, wanaume 18 na vifo vya watu 13 wanawake sita, wanaume saba.

“Shirika linaendelea kuwasihi madereva wa vyombo vya moto kufuata sheria na alama za usalama katika njia ya reli na barabarani zilizowekwa ili kuepusha ajali.

“Shirika linatoa pole kwa ndugu wa marehemu na Mwenyezi Mungu awape nafuu majeruhi waweze kuendelea na shughuli za kujenga taifa,” imesema taarifa hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Habari Mchanganyiko

TMA yapongezwa kuimarisha ubora na usahihi wa taarifa za Hali ya Hewa

Spread the love  WAFANYAKAZI wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA),...

error: Content is protected !!