Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko 11 waliomuua Wayne Lotter wahukumumiwa kunyongwa
Habari Mchanganyiko

11 waliomuua Wayne Lotter wahukumumiwa kunyongwa

Kitanzi
Spread the love

 

MAHAKAMA Kuu kanda ya Dar es Salaam leo tarehe 2 Disemba, 2022 imewahukumu adhabu ya kunyongwa hadi kufa watu 11 waliokutwa na hatia ya kumuua mwanaharakati wa ujangili, raia wa Afrika Kusini, Wayne Lotter. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Jaji wa Mahakama Kuu Laila Mgonya ametoa hukumu hiyo baada ya kuridhika na ushahidi wa mashtaka uliothibitishwa pasina shaka na mashahidi 32.

Waliohukumiwa ni raia wawili wa Burundi Nduimana Ogiste na Habonimanda Nyandwi pamoja na Watanzania Godfrey Salamba, Rahma Almas,  Chambie Juma Ally, Allan Mafue, Ismail Mohammed, Leonard Makoi, Ayoub Kiholi, Abuu Mkingie, Muchael Kwavava.

Wayne Lotter

Lotter alikuwa Mkurugenzi na Mwanzilishi-mwenza wa Shirika lisilo la kiserikali la PALMS Foundation lilokuwa likijihusisha na mapambano ya ujangili.

Aliuawa tarehe 16 Agosti, 2017 kwa kupigwa risasi na watu waliomvamia akiwa kwenye gari ndogo ya abiria ‘texi’ katika makutano ya barabara za Chole na Haile Selaissie, Masaki wilayani Kinondoni mkoani Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!