Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Happines Sanga awa mwanafunzi bora ARU
Elimu

Happines Sanga awa mwanafunzi bora ARU

Spread the love
WANAFUNZI 96 wa Chuo Kikuu Ardhi (ARU),   wametunukiwa tuzo mbalimbali kutokana na kufanya vizuri kitaaluma kwa mwaka wa masomo 2021/22. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Wanafunzi hao walikabidhiwa tuzo hizo leo chuoni hapo na Makamu Mkuu wa chuo hicho, Profesa Evaristo Liwa, kwenye hafla fupi ya kuwapongeza wanafunzi hao.

Mwanafunzi wa kike alibuka mshindi wa jumla ni Happiness Sanga.

Akizungumza kwenye hafla hayo, Naibu Makamu Mkuu wa Chuo, Taaluma, Utafiti na Ushauri, Profesa John Lupala alisema sherehe za kuwazawadia wanafunzi hao kila mwaka zimekuwa zikiwezeshwa na wadau mbalimbali.

Aliwapongeza wadau hao na kuwaomba waendelee kuunga mkono jitihada za wanafunzi hao kwani zawadi mbalimbali zinazotolewa na wadau hao zimekuwa zikisaidia kuongeza ari ya utendaji kazi kwa wanafunzi.

Profesa Lupala alisema tuzo hizo zimekuwa zikisaidia sana kuongeza tija kwenye maisha ya wanafunzi ya kielimu na kiuchumi huko wanakokwenda kufanyakazi.

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Ardhi (ARU), Profesa Evaristo Liwa akimpa cheti mwanafunzi bora wa mwaka huu wa masomo Happiness Sanga

“Kwenye sherehe za mwaka huu tuna wanafunzi 96, kati yao wasichana ni 50 na wavulana ni 46 ambao wamefuzu kupata tuzo na zawadi mbalimbali kwa vipengele mbalimbali vya kitaaluma,” alisema Profesa Lupala.

Aliwapongeza wanafunzi wote waliopokea tuzo hizo na kuwataka waendelee kuweka jitihada kwenye masomo yao ili waje kuwa mfano wa kuigwa kwa wanafunzi wenzao na jamii kwa ujumla.

Kwa upande wake Makamu Mkuu wa Chuo, Profesa Liwa alisema sherehe za utoaji tuzo Chuoni hapo zitafuatiwa na shughuli ya Mahafali siku ya Jumanne tarehe 6 Desemba ambapo wahitimu 930 wa ARU wa Shahada mbalimbali watatunukiwa Stashahada zao na aliwapongeza kwa kufikia hatua hiyo muhimu kwenye maisha yao.

“Nawapongeza sana wahitimu na baadhi yao wamekuwa wakipokea tuzo mbalimbali kwa miaka kadhaa mfululizo hii inamaanisha kwamba kwenye juhudi ya kweli mafanikio hupatiana ni matumaini ya chuo kuwa juhudi hizo mtaziendeleza kwenye shughuli za ujenzi wa taifa,” alisema

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Ardhi (ARU), Profesa Evaristo Liwa akimpa cheti mmoja wa wanafunzi wanaohitimu Jumanne

Aliwataja baadhi ya wadau waliotoa tuzo hizo kuwa ni Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Bodi ya Wathamini Tanzania (VRB), Bodi ya Usajili wa Wabunifu na Ukadiriaji Ujenzi (AQRB), African Property Limited, Taasisi ya Wabunifu na Wakadiriaji Ujenzi (TIQS), Mekon na Webb Uronu and Partners.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

error: Content is protected !!