KLABU ya Simba imeitaka Kamati ya Sheria na Hadhi ya Wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) mpaka kufikia Machi 24, 2017, iwe imeshatoa maamuzi waliyoyaweka kiporo, kinyume na hapo watachukua maamuzi magumu, anaandika Erasto Masalu.
Simba wametoa kauli hiyo baada ya kuwepo kwa sintofahamu juu ya maamuzi ya Kamati ya Usimamizi na Uendeshaji wa Ligi (Kamati ya masaa 72) ya kuipa pointi tatu kutokana na rufaa yao dhidi ya Kagera Sugar kumchezesha Mohammed Fakhi.
Haji Manara,Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano klabu ya Simba SC amewaambia waandishi wa habari kuwa anashangazwa na watani wao wa jadi kushikia bango suala hilo ili hali likiwa haliwahusu.
Manara, amesema hawatishwi na wapinzani wao waliosema wanamwaga mboga kuhusiana na kupewa pointi 3 dhidi ya Kagera Sugar na sasa kama vipi wao watabutua sahani na bakuli wakose wote.
“Juzi kiongozi mmoja wa Yanga ameongea na vyombo vya habari na kuitishia TFF kwamba wameenda TAKUKURU na Polisi kuomba wafanya uchunguzi juu ya maamuzi ya kamati ya saa 72, baadae TFF wanaitisha kikao cha Kamati ya Sheria na Hadhi za wachezaji kupitia maamuzi yaliyotolewa na kamati ya saa 72,” amesema Manara.
Amesema mkwara wa Yanga umewatisha sana TFF na kuanza kufanya vitu ambavyo kimsingi vilikuwa vimeshaisha. TFF inaonekana kuipendelea Yanga kwa kila jambo.
Aidha Manara amesema, Kamati hiyo ya Sheria na Wachezaji mpaka leo haijatoa maamuzi juu ya suala ya Tambwe dhidi ya Juuko? mwaka wa pili unamalizika, Banda kampika ngumi Kavilla ndani ya wiki moja uamuzi umeshatolewa, hii kamati tunashindwa kuielewa?
Kagera kukata rufaa dhidi ya Simba ndani ya wiki wameshakaa kikao kupitia taarifa, huu ni upendeleo wa wazi kabisa na hawawezi kukubali TFF kuwa inawabeba upande mmoja tu.
Spread the love MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...
By Mwandishi WetuApril 26, 2024Spread the love LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...
By Mwandishi WetuApril 24, 2024Spread the love NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...
By Mwandishi WetuApril 24, 2024Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...
By Mwandishi WetuApril 24, 2024
Leave a comment