Monday , 5 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Vyama vya wafanyakazi wakumbushwa kanuni
Habari Mchanganyiko

Vyama vya wafanyakazi wakumbushwa kanuni

Wafanyakazi wa kiwanda cha maziwa cha Azam wakiwa kazini
Spread the love

SERIKALI imewataka watendaji wa vyama vya wafanyakazi kuzisoma, kuzitambua na kuzitumia vyema kanuni na sheria za kazi ili kutatua migogoro ya wafanyakazi na waajiri bila upendeleo na kuleta tija kwa Taifa, anaandika Christina Haule.

Wito huo ulitolewa jana na Kamishna wa kazi, Hilda Kabisa wakati akifungua mkutano wa watendaji wa vyama vya wafanyakazi na waajiri kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Erick Shitindi uliofanyika mkoani Morogoro.

Kabisa amesema kufuatia kuwepo kwa malalamiko ya wafanyakazi ya madai kuwa watendaji wa vyama vya wafanyakazi wanatatua migogoro ya wafanyakazi dhidi ya waajiri kwa kuwapendelea waajiri bila kukumbuka kuwa wanatakiwa kutenda wajibu wao bila upendeleo ni wazi kuwa viongozi hao wamezisahahu kanuni na sheria za kazi ambazo wanapaswa kuzifuatwa ili kuleta amani.

“Kama kutakuwa na upendeleo upande mmoja wakati wa utatuzi wa migogoro ya wafanyakazi, hakutakuwa na amani,” amesema Kabisa.

Amesema watendaji wa vyama vya wafanyakazi wanapaswa kutimiza wajibu wao, kwani wao ni kiungo sahihi kwa wafanyakazi na waajiri ili kukuza uchumi wa nchi.

Naye Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Malori Tanzania, Greyson Unile amesema elimu inapaswa kutolewa kwa wafanyakazi na waajiri ili kuweza kutatua changamoto zinazowakabili wote kwa pamoja na kufanya kushindwa kutekeleza wajibu wao vyema sehemu za kazi.

Unile amesema, zipo changamoto za uelewa wa namna ya kutekeleza masuala ya ajira mahala pa kazi kwa waajiri kufuatia waajiri kutokubali kutekeleza sheria huku wakiwaona watendaji wa vyama vya wafanyakazi kuwa ni adui na sio wazuri kwao.

Amesema, yapo masuala ya kazi ambayo wafanyakazi wanapaswa kuyazingatia ili kuboresha suala la ajira na kwamba wafanyakazi wameonekana kutoyazingatia kutokana na uelewa mdogo.

Hata hivyo Katibu msaidizi wa chama hicho, Yasini Kabingwa ameishauri serikali kuongeza bajeti ya wizara hiyo ili elimu iweze kutolewa na kuimarisha nafasi za watendaji sababu kufuatia maofisa wa kazi kuwa wachache katika mikoa hufanya huduma kushindwa kutolewa vyema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

Habari Mchanganyiko

Bandari ya Kigoma kuongezewa uwezo wa kutoa huduma zake

Spread the love  SERIKALI kupitia mamlaka ya Bandari nchini (TPA), imewekeza takribani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kifo cha mwanafunzi UDOM: Tume yamsafisha naibu waziri

Spread the loveTUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini (THBUB),...

error: Content is protected !!