Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wauaji wa Kibiti wahofiwa kujificha Dar
Habari Mchanganyiko

Wauaji wa Kibiti wahofiwa kujificha Dar

Simon Sirro, Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam
Spread the love

SIMON Sirro, Kamishna wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, amewataka wakazi wa jiji hilo kuwa makini hasa katika kipindi hiki uchunguzi dhidi ya waliotekeleza mauaji ya askari nane, Kibiti, Pwani, anaandika Hamisi Mguta.

Rai hiyo ameitoa leo ofisini kwake kufuatia msako uliodaiwa kuwa mkali kwa majambazi walioshiriki mauaji hayo huku akiwataka madereva bodaboda kuwa makini na abiria wanaowabeba.

“Watu hawa wengi naamini wamekimbilia Dar es Salaam, sina maana ya kuwatia hofu lakini Dar es Salaam na Pwani tunaingiliana sana na mtu akijificha huku inakuwa ni ngumu sana kumpata kama huwezi kuwa na ujanja wa kutosha,” amesema Kamanda Sirro.

Amefafanua kuwa ni vizuri madereva hao wakajenga utaratibu wa kuwa na viongozi ambao watasimamia usalama kwa kuchukua namba ya simu ya abiria na hata wakati mwingine ikiwezekana akapiga picha mtu mnayemtilia mashaka.

“Muda ambao unajua ni mbaya anakuja mteja anataka umpeleke mahala fulani, na unajua ni pori ni lazima ujiulize, maanake wengine kwenye vijiwe unakuta hawapendani na najua kuna watu wanaendesha boda boda kwa ajili ya kufanya uhalifu,” amesema.

Wakati huo huo amewaambia waaandishi wa habari kuwa mnamo Aprili, 15 majira ya 07;00 usiku maeneo ya Kiwalani kwa Ally Mboa, Jeshi hilo limekamata silaha moja aina ya ‘shotgun’ ambayo imekatwa kitako na mtutu na huku namba zake zikiwa zimefutwa.

“Silaha ilipatikana wakati askari wa doria wakiwa katika maeneo hayp ambapo walihisi harufu ya bangi na kuanza kufuatilia ili kubaini ndipo ghafla watu wawili wasiofahamika walikurupuka na kupanda pikipiki (haikusomeka namba) kisha kuangusha begi lenye ambalo lilibainika kuwa na silaha,” amesema.

Aidha katika kuipekua zaidi walikuta risasi nne zikiwa zimefungwa kwenye mfuko wa plastiki pamoja na jaketi jeusi na kofia.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!