Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wauzaji kuku Singida wapaza sauti
Habari Mchanganyiko

Wauzaji kuku Singida wapaza sauti

Kuku wa kienyeji
Spread the love

WAFANYABIASHARA wa soko la kuku mkoani Singida wameiomba Serikali kuangalia na kuboresha upatikanaji wa masoko ya uhakika hapa nchini, anaandika Christina Haule.

Ombi hilo lilitolewa na Mwenyekiti wa soko hilo, Shabani Mahiki wakati akizungumza na viongozi na waandishi kutoka klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Morogoro (MoroPC) na Singida SingPress walipotembelea kwenye soko hilo kuona faida na manufaa wanayopata wafanyabaishara hao.

Mahiki alisema wafanyabiashara wanaosafirisha kuku kwenye matenga kwenda mkoa mbalimbali hasa jijini Dar es salaam wanunuzi wamekuwa siyo waaminifu.

“Utakuta mmetuma mzigo labda tenga zenye thamani ya shilingi milioni moja halafu mtu anapokea mzigo na baada ya wiki kadhaa anakutumia laki tano badala ta kukutumia zote,” amesema Mahiki.

Muuzaji wa kuku katika soko hilo, Jumanne Mkotya aliiomba Serikali kuondoa au kufuta ushuru kwa biashara ya kuku.
Mkotya amesema, usafirishaji wa kuku mikoani husababisha baadhi ya kuku kufa njiani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!