Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Watu 60 mbaroni kwa kuharibu miundombinu ya Tanesco
Habari Mchanganyiko

Watu 60 mbaroni kwa kuharibu miundombinu ya Tanesco

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa
Spread the love

ZAIDI ya watu 60 wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa tuhuma za uharibifu wa miundombinu ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Hayo yamesemwa leo tarehe 2 Oktoba 2018 na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamanda Lazaro Mambosasa wakati akizungumza na wanahabari.

Kamanda Mambosasa amesema watuhumiwa hao wamekamatwa katika nyakati tofauti kwenye operesheni za kusaka waharibifu wa miundombinu ya shirika hilo, zinazoendeshwa na TANESCO kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi.

Sambamba na watuhumiwa hao, Kamanda Mambosasa amesema Jeshi la Polisi linamshikilia dereva bodaboda mmoja anayefahamika kwa jina la Matthew Joseph kwa kosa la kumiliki na kuitumia katika matukio ya kihalifu, bunduki aina ya shotgun.

Amesema watuhumiwa hao wanaendelea na mahojiano na kwamba yakikamilika watachukuliwa hatua za kisheria zaidi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!