Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wajasiriamali waanika kinachoua VICOBA
Habari Mchanganyiko

Wajasiriamali waanika kinachoua VICOBA

Spread the love

WAJASIRIAMALI wilaya ya Temeke mkoa wa Dar es Salaam, wameeleza sababu zinazopelekea vikundi vya kuweka akiba na kukopa mikopo kufa na kuacha maumivu kwa wanachama walioweka fedha zao. Anaripoti Mwandishi Wetu  … (endelea).

Akizungumza katika mkutano wake na wanachama wa vikundi vya VICOBA Endelevu wilayani humo, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanawake Temeke, Johari Mkonde amesema miongoni mwa sababu za vikundi hivyo kufa ni pamoja na usimamizi mbovu kuhusu masuala ya fedha na ukiukiwaji wa katiba za vyama hivyo.

Johari ambaye pia ni Mratibu wa Taasisi ya VICOBA Endelevu-SDA, amesema kitendo cha baadhi ya wanachama kutolipa mikopo yao kwa wakati na wengine kukimbia na fedha za vikundi, ni miongoni mwa sababu za vikundi hivyo kutotimiza malengo yake na hatimaye kuvunjika.

“Ulipaji wa mikopo umekuwa changamoto kubwa. Wasimamizi wa mikopo wanatakiwa kutowalea wanaogoma kulipa mikopo kwa wakati, inatakiwa wahakikishe waliokopa wanalipa madeni yao kwa wakati ili hizo fedha ziwanufaishe wanachama wengine,” amesema na kuongeza Johari.

“Kikundi kikishirikiana katika kufuatilia ulipaji wa madeni, wanaokopa hawawezi kukimbia na pesa, inatakiwa tuwe na msimamo ili tuweze kufikia malengo ya kujikwamua kiuchumi. Wale wanaohusika na marejesho waendelee na majukumu yao.”

Katika hatua nyingine, Johari amewahimiza wajasiriamali kusajili vikundi vyao vya kuweka akiba na kukopa mikopo serikalini, ili viweze kutambulika na kupata fursa zinapojitokeza

Johari ameeleza kwamba, changamoto ya wajasiriamali kutosajili serikalini vikundi vyao, imepelekea kutotambulika pindi fursa zinapojitokeza, na kuwataka wanachama wa vikundi hivyo kufuata taratibu na masharti ya usajili, ili wasajili vikundi vyao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!