Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wabunge walioko Dar watakiwa kujisalimisha Polisi
Habari za Siasa

Wabunge walioko Dar watakiwa kujisalimisha Polisi

Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Polisi Dar es Salaam
Spread the love

JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam nchini Tanzania, limewataka wabunge waliokaidi agizo la kurejea bungeni jijini Dodoma ndani ya masaa 24, kujisalimisha Ofisi ya Upelelezi ya kanda hiyo, kwa ajili ya mahojiano. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Jana Jumatano tarehe 6 Mei 2020, Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, aliwataka wabunge wasiokuwa na vibali vya udhuru kutoka kwa Spika Job Ndugai, kurejea bungeni kwa ajili ya kuhudhuria vikao vya bunge vinavyoendelea.

Leo tarehe 7 Mei 2020, SACP Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, amewataka wabunge hao kwa hiari yao kuripoti Ofisi ya Upelelezi ya kanda hiyo mara moja.

Taarifa ya agizo hilo la Kamanda Mambosasa, limetolewa kwa niaba yake na kamanda Ronarl K. Makona.

“Kufuatia agizo la Mkuu wa Mkoa na Mwenyekiti Wa Kamati ya Ulinzi na Usalama mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la tarehe 6 Mei 2020, kwa waheshimiwa wabunge ambao wapo mkoani hapa badala ya kuwa bungeni Dodoma, kurudi ndani ya saa 24,” inaeleza taarifa ya Kamanda Makona kwa niaba ya Mambosasa.

Taarifa hiyo imeongeza, “Kwa wale ambao bado wapo jijini Dar es Salaam wanatakiwa kuripoti kwa hiari yao Ofisi ya Upelelezi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kwa mahojiano.”

Agizo la Makonda alilitoa kipindi ambacho baadhi ya wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wanaendelea kutekeleza maagizo ya chama hicho yaliyotolewa na Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema tarehe 1 Mei 2020 la kuwataka kutohudhuria shughuli za bunge na wabaji majumbani mwao kwa siku 14 kujikinga na maambukizi ya corona.

Hatua hiyo ilitokana na vifo vya wabunge watatu vilivyotokea ndani ya wiki mbili akiwamo waziri wa katiba na sheria, Balozi Augustine Mahine. Wengine waliofariki ni Getrude Rwakatare, mbunge wa viti maalum pamoja na Richard Ndassa mbunge wa Sumve.

Mbowe aliwataka wabunge hao wakae karantini, hadi pale janga hilo litakapopatiwa ufumbuzi wa namna ya kudhibitiwa.

Pia, Mbowe alilitaka bunge lisitishe shughuli zake, kisha kuwapima wabunge wote na watumishi wa mhimili huo, ili kujua hali ya maambukizi ya ugonjwa huo, pamoja na kupata ufumbuzi wa kudhibiti ueneaji wake.

Lakini hatua hiyo ilipingwa na Makonda kwa madai kwamba, wabunge hao hawawatendei haki wawakilishi wao kwa kutohudhuria bungeni, huku akiwafananisha na wazurulaji.

Makonda alisema wabunge hao wasiporudi bungeni ndani ya saa 24, watakamatwa kwa kosa la uzururaji.

“Hakuna asiyefahamu kuwa sasa hivi tuko katika mapambano dhidi ya virusi vya Corona na sio uzururaji, ifahamike huu sio mji wa wazururaji hivyo natoa saa 24 kwa wabunge wote kurudi Dodoma tofauti na hapo tutawakamata kwa kosa la uzururaji kama tunavyowakamata machangudoa,” amesema Makonda.

Tangu kutolewa kwa agizo hilo la Makonda, baadhi ya wabunge akiwamo Zitto Kabwe wa Kigoma Mjini kupitia ACT-Wazalendo walilipingwa na kudai katiba ya Tanzania inawaruhusu kuwa eneo lolote lile bila kubughudhiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!