Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Uhujumu uchumi: Kigogo mwingine ajitosa kwa DPP
Habari za Siasa

Uhujumu uchumi: Kigogo mwingine ajitosa kwa DPP

Kuluthum Mansoor, akiwa mahakamani wakati wa kesi yake
Spread the love

KULUTHUM Mansoor, aliyekuwa Mkurugenzi wa Mipango, Ufuatiliaji na Tathimini wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), amekiri kosa na kutaka yaishe. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Elia Mwingira, Wakili wa Utetezi ameiambia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kwamba wameandika barua kwenda kwa Mkurugenzi wa Makosa nchini (DPP) Biswalo Mganga kukiri makosa ya Kuluthum.

Kigogo huyo wa Takukuru anakabiliwa na mashtaka manane likiwemo la utakatishaji fedha kiasi cha Sh. 477 Bil. Mashitaka mengine ni kughushi, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Wakili wa Kuluthum ametoa kauli hiyo baada ya Wankyo Simon, wakili wa serikali mwandamizi kudai mahakamani hapo kuwa, upelelezi haujakamilika.

Hata hivyo, wakili Mwingira ameiomba mahakama kuzingatia kwamba, mteja wake tayari ameandika barua hiyo kwa lengo la kutaka apatiwe haki yake ya msingi.

Pamoja na maelezo hayo, Hakimu Mfawidhi, Kelvin Mhina ameahirisha shauri hilo mpaka tarehe 16 Oktoba 2019 itakapotajwa tena.

Jumapili ya tarehe 22 Septemba 2019, Rais John Magufuli alishauri ofisi ya DPP, kwamba wale wenye kesi za uhujumu uchumi na utakatishaji fedha, kama wapo tayari kuomba radhi na kurejesha fedha, ofisi hiyo iangalie utaratibu wa kuwaachia ndani ya siku saba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!