Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Tundu Lissu atinga kwa Obama
Habari za SiasaTangulizi

Tundu Lissu atinga kwa Obama

Spread the love
MWANASHERIA mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, amewasili jijini Washington, nchini Marekani ili kuzungumza katika mdahalo wa aina yake katika chuo kikuu cha George Washington. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Katika ziara hiyo, Lissu ameongoza na mkewe, Alicia Magabe.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa watu waliokaribu na mwanasiasa huyo na chama chake jijini Dar es Salaam zinasema, Lissu atashiriki katika mjadala wa moja kwa moja unaozungumzia, “Tanzania’s Democratic Challenge,” utakaofanyika kwenye chuo kikuu cha George Washington.

Aidha, katika ziara hiyo, Lissu atapata nafasi ya kushiriki mjadala utakaongozwa na  Jenniffer Cooke, mkurugenzi wa taasisi ya Instute for African Studies (IAfS). Lissu atakuwa mgeni mwalikwa.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, katika ziara hiyo, Lissu anatarajiwa kukutana na Rais mstaafu wa Marekani, Barack Obama. 

Lissu ambaye yuko nchini Ubelgiji kwa matibabu yanayotokana na kushambuliwa kwa risasi, yuko kwenye ziara ya nchi kadhaa za Ulaya na Marekani, kueleza kile anachokiita, “kinachoendelea nchini kuhusu demokrasia na utawala wa sheria.”

Mwanasiasa huyo ambaye pia ni mbunge wa Singida Mashariki na Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni, alishambuliwa na watu “wasiojulikana” akiwa ndani ya gari lake, alipokuwa akirejea nyumbani kwake kutokea bungeni, eneo la Area D, mjini Dodoma.

Tukio hilo lililotokea tarehe 7 Septemba mwaka 2017.

Kabla ya kupelekwa Ubelgiji, Lissu alipata matibabu katika hospitali ya mkoa wa Dodoma na baadaye Nairobi nchini Kenya.

Mpaka sasa, hakuna mtu yeyote ambaye amekamatwa kutokana na shambulio hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!