Katika ziara hiyo, Lissu ameongoza na mkewe, Alicia Magabe.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa watu waliokaribu na mwanasiasa huyo na chama chake jijini Dar es Salaam zinasema, Lissu atashiriki katika mjadala wa moja kwa moja unaozungumzia, “Tanzania’s Democratic Challenge,” utakaofanyika kwenye chuo kikuu cha George Washington.
Lissu ambaye yuko nchini Ubelgiji kwa matibabu yanayotokana na kushambuliwa kwa risasi, yuko kwenye ziara ya nchi kadhaa za Ulaya na Marekani, kueleza kile anachokiita, “kinachoendelea nchini kuhusu demokrasia na utawala wa sheria.”
Mwanasiasa huyo ambaye pia ni mbunge wa Singida Mashariki na Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni, alishambuliwa na watu “wasiojulikana” akiwa ndani ya gari lake, alipokuwa akirejea nyumbani kwake kutokea bungeni, eneo la Area D, mjini Dodoma.
Tukio hilo lililotokea tarehe 7 Septemba mwaka 2017.
Kabla ya kupelekwa Ubelgiji, Lissu alipata matibabu katika hospitali ya mkoa wa Dodoma na baadaye Nairobi nchini Kenya.
Mpaka sasa, hakuna mtu yeyote ambaye amekamatwa kutokana na shambulio hilo.
Leave a comment