Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Switzerland yawakumbuka walemavu
Habari Mchanganyiko

Switzerland yawakumbuka walemavu

Spread the love

WATU wenye ulemavu nchini wameiomba serikali  na taasisi mbalimbali binafsi kuwasaidia  eneo la   kujenga ofisi ya kudumu. Anaandika Angela Willium

Wamesema wanahitaji ofisi kwa kuwa hivi sasa sehemu wanayotumia wameazimwa kwa muda na Msikiti wa Membe Chai uliopo jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam,  Mwenyekiti wa Taasisi  ya Walemavu ijulikanayo kama MITWE, Habibu Hamimu amesema tatizo hilo la kukosa ofisi wamekuwa nalo kwa muda mrefu sasa.

Aliyasema hayo wakati akipokea msaada wa viti vya walemavu na baiskeli kutoka Taasisi ya Furaha ya Switzerland.

“Tunaiomba serikali na wana  jamii watusadie eneo la kujenga ofisi ya kudumu  kwani hapa tulipo ni jengo la Msikiti wa   Mwembechai ambayo hata hivyo  hiyo inavuja kipindi cha mvua na misaada tuyopokea ni mikubwa ikilinganisha na ofisi tuliyo nayo, ” amesema Hamimu

Kwa upande wake, Katibu wa chama hicho  wilaya ya Kinondoni,   Saidi Machaku amesema walemavu wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo suala la afya.

“Wazazi au walezi wanao ishi na watu wenye ulemavu tuna waomba muwe mna waleta walemavu wenzetu katika kupokea misaada badala ya kuwafungia ndani na hapa kuna mlemavu mmoja sijamuona nahisi wazazi hawajamleta kwa kuwa wanaona aibu kuja naye, ” amelalamika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!