Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Shamba la Rais Kikwete lavamiwa
Habari MchanganyikoTangulizi

Shamba la Rais Kikwete lavamiwa

Rais Jakaya Kikwete na Mama Salma akiwa shambani
Spread the love

MBUNGE wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete amesema shamba la baba yake, Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete lililoko kata ya Kibindu wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani, lilivamiwa na mfugaji mwenye ng’ombe wasiopungua 800. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Ridhiwani ameyasema hayo leo tarehe 26 Oktoba 2018 mbele ya Makamu wa Rais, Samia Suluhu wakati akizungumzia kuhusu changamoto ya uvamizi wa maeneo unaofanywa na baadhi ya wafugaji wa kuhama hama, katika mkutano wa hadhara uliofanyika jimboni kwake, Chalinze.

Akielezea kuhusu tukio hilo, Ridhiwani amesema amebaini uvamizi huo baada ya kwenda shambani huko na Afisa Polisi wa Chalinze wiki tatu zilizopita, na kumkuta mfugaji huyo anayetokea mkoani Manyara, akilisha ng’ombe hao.

“Mfano mmoja ulio hai, wiki tatu zilizopita kamanda wangu wa polisi wa hapa Chalinze nilikwenda nae Kibindu, na ili kujua hii hali imekuwa mbaya kuna mfugaji mmoja kutoka Manyara amekwenda kuvamia shamba la rais mstaafu, amekwenda kuweka ndani ng’ombe wasiopungua 800, kama sio elfu moja na anasema kabisa kwamba kama hajalisha pale akalishe wapi,” amesema na kuongeza Ridhiwani.

“Wakati mwingine sisi kwa nafasi zetu kama wabunge tunaogopa hata kutumia nguvu kwa sababu zile mali nyingine ni mali binafsi, ninaamini haya yanaweza kutatuka kama wizara yetu ya kilimo mifugo itaweka mguu.”

Akizungumzia kuhusu changamoto hiyo, Mama Samia amesema serikali itafanyia kazi suala hilo ili kuhakikisha wafugaji wanaofuga kwa kuhama hama hawavamii maeneo ya watu.

“Kwenye Suala la ufugaji wa kuhama hama na kuvamia maeneo, nashukuru sana aibu waziri mifugo na uvuvi amelitolea ufafanuzi mzuri, lakini niahidi serikali italisimamia,” amesema Mama Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!