Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Safari za mabasi usiku zapigwa ‘stop’
Habari Mchanganyiko

Safari za mabasi usiku zapigwa ‘stop’

Spread the love

JESHI la Polisi limetangaza kusitisha safari za usiku kwa baadhi ya magari ya abiria yanayokwenda mikoani. Anaripoti Hamis Mguta…(endelea).

CP Liberatus Sabas, Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa jeshi hilo amesema, wameamua kuchukua hatua hiyo kutokana na sababu za kiusalama na kuwa, mabasi yatakayoruhusiwa kufanya safari zake za usiku ni  Morogoro -Dar es Salaam, Shinyanga – Mwanza pekee.

Amesema, mabasi ambayo hayataruhusiwa kufanya safari zake usiku ni Dar es Salaam-Kahama-Mwanza, Dar es Salaam-Tabora-Katavi, Kahama- Geita-Kagera, Kahama kwenda mikoa mingine iliyopo mipakani pamoja na Dar es Salaam-Tabora kwenda katika wilaya zake.

“Jeshi la Polisi limejipanga kikamilifu kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama, kulifanyia kazi suala la usalama na baadaye mabasi yote yataruhusiwa kutembea usiku,” amesema.

Kwa mujibu wa CP Sabas ni kwamba, zoezi la kuzuia mabasi hayo kusafiri usiku limeanza kutekelezwa kabla ya taarifa hizo kutolewa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!