RAISI wa Madktari nchini Dk.Elisha Osati, ameiomba serikali kuongeza mishahara kwa watumishi wanaotoa huduma kwenye sekta ya afya nchini ili kumudu mahitaji ya maisha. Anaripoti Faki Sosi, (endelea).
Akizungumza na MwanaHALISI ONLINE Dk. Elisha Osati amesema kuwa, kwa sasa serikali inatoa mishahara kwa wakati.
“Kwa sasa tunapata mishahara kwa muda muafaka labda kwa waajiriwa wapya ambao pia wanapata mishahara yao kwa muda tu ingawa kunachangamoto ndogondogo,” amesema.
Na kwamba, licha ya mishahara kulipwa kwa wakati ameeleza kuwa, bado kiwango cha mishahara hiyo haiendani na namna wanavyoitumikia kada hiyo.
“Kwa kweli mishahara haitoshi hivyo nafikiri ukiongea na daktari yoyete au mafanyakazi yoyete wa sekta ya afya, atakwambia mishahara haitoshi kwa namna tunavyofanya kazi na muda tunaotumia kutoa huduma za afya,” amesema Dk Osati na kuongeza;
“Bado tunaiomba Serikali na tunaamini bado inanafasi ya kuongeza mishahara lakini sio serikali tu hata mashirika binafsi hospital, binafsi ambayo kuna madaktari bado tunaomba lipokewe hilo sisi kama chama cha madakrari tunaangalia weledi wa kitaaluma wa madaktari na huwezi kuzungumzi weledi bila kuzungumzia ustawi wa madaktari”.
Amesema kuwa, amemshukuru Rais John Magofuli na Serikali yake kwa kujali kada hiyo ikiwa pamoja kwa kushughulikia matatizo ya madakri kwa muda muafaka.
Tazama video kamili hapo chini
Leave a comment