Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Mwinyi aanza kuunda serikali. ateua AG
Habari za Siasa

Rais Mwinyi aanza kuunda serikali. ateua AG

Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Mwinyi
Spread the love

RAIS wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi ameanza kuisuka Serikali anayoiongoza kwa kumteua Dk. Mwinyi Twalib Haji kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG). Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Dk. Mwinyi amefanya uteuzi huo jana Jumanne tarehe 3 Novemba 2020 ikiwa ni siku moja imepita tangu alipoapishwa kuwa Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar.

Huu ni uteuzi wa kwanza kuufanya mara baada ya kuingia Ikulu ya Zanzibar.

Kabla ya uteuzi huo, Dk. Haji alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Dk. Mwinyi aliapishwa juzi Jumatatu tarehe 2 Novemba 2020 na Jaji Mkuu wa Zanzibar, Omar Othuman Makungu akichukua nafasi ya Dk. Ali Mohamed Shein ambaye amemaliza muda wake wa uongozi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!