RAIS wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi ameanza kuisuka Serikali anayoiongoza kwa kumteua Dk. Mwinyi Twalib Haji kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG). Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Dk. Mwinyi amefanya uteuzi huo jana Jumanne tarehe 3 Novemba 2020 ikiwa ni siku moja imepita tangu alipoapishwa kuwa Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar.
Huu ni uteuzi wa kwanza kuufanya mara baada ya kuingia Ikulu ya Zanzibar.
Kabla ya uteuzi huo, Dk. Haji alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Dk. Mwinyi aliapishwa juzi Jumatatu tarehe 2 Novemba 2020 na Jaji Mkuu wa Zanzibar, Omar Othuman Makungu akichukua nafasi ya Dk. Ali Mohamed Shein ambaye amemaliza muda wake wa uongozi.
Leave a comment