Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli: Kuna wakati Waziri Ummy alitengwa
Habari za Siasa

Rais Magufuli: Kuna wakati Waziri Ummy alitengwa

Ummy Mwalimu, Waziri wa TAMISEMI
Spread the love

UMMY Mwalimu, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto amewashangaa wale wote waliokuwa wakihoji alipo Rais wa Tanzania, John Magufuli katika mapambano ya ugonjwa unaosababishwa na virusi vya corona (COVID-19). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea)

Waziri Ummy amesema katika kipindi hiki cha mapambano ya corona, amejifunza mengi ikiwemo maelekezo mbalimbali aliyokuwa akiyapata kutoka kwa Rais John Magufuli ambaye alikuwa nyumbani kwake, Chato mkoani Geita.

Rais Magufuli alikuwa Chato kwa zaidi ya mwezi mmoja hadi jana Jumatano tarehe 20 Mei, 2020 aliporejea Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma.

Waziri Ummy, akizungumza katika hafla kuapishwa kwa viongozi sita aliowateua akiwamo Dk. Godwin Mollel kuwa naibu waziri wa afya kuchukua nafasi ya Dk. Faustine Ndungulile amempongeza Rais Magufuli kwa uongozi wake.

“Dk. Mollel umekuja kipindi hiki tunapambana na corona, kubwa ni kuwatoa hofu na Watanzania wengi walikuwa wanaumwa hofu,” amesema Waziri Ummy.

Amesema, wagonjwa wamepungua sana katika hospitali huku akigusia jinsi walivyokuwa wameandaa vitanda 1,000 kwenye viwanja vya saba saba jijini Dar es salaam ili kuwalaza lakini kutokana na kupungua kwa wagonjwa, wamesitisha mpango huo.

“Kuna watu walikuwa wanasema (Rais Magufuli) hawakuoni, lakini katika kipindi hiki chenye changamoto, nilikuwa napata maelekezo mengi kutoka kwako. Ukiniona mimi umemwona Rais Magufuli,” amesema Waziri Ummy huku akifurahia pamoja na Rais Magufuli mwenyewe.

Rais John Magufuli

Waziri Ummy amesema, uongozi wa Rais Magufuli umesaidia kuimarisha sekta ya afya na hakuna halmashauri yoyote nchini ambayo haijaguswa ikiwamo ujenzi wa hospitali na vituo vya afya.

Amesema huduma zimeboreshwa ikiwamo kupunguza wagonjwa kupelekwa nje ya Tanzania.

Naye, Rais Magufuli amesema, “waziri wa afya anajituma kweli kweli, katika suala hili la corona alisimama kweli. Kuna wakati fulani nilikuwa namwona kama yuko peke yake kwenye wizara.”

Amesema Waziri Ummy siyo mtaalamu wa afya, wasaidizi wake wote ni wataalamu lakini walimwacha, “nilikutesa kweli. Kuna wakati nilimpigia simu zaidi ya mara nane, hadi uisku. Katika vita, kuna wakati hupaswi kubembelezana.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!