PROFESA Palamaganda Kabudi, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, amewataka watumishi wa umma nchini kuwa waadilifu na uaminifu wakiwa kwenye majukumu yao. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Kabudi amesema hayo leo Jumatatu tarehe 6 Julai 2020 Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma kwenye hafla ya Rais John Pombe Magufuli kuapisha viongozi mbalimbali aliowateua hivi karibuni.
Kabudi amesema vyeo walivyopewa ni dhamana yenye thamani mbele ya Mwenyezi Mungu.
“Sisi sote ambao tumepewa dhamana kubwa ya kuwaongoza Watanzania, tujue hakuna kazi ya thamani kubwa machoni mwa Mwenyezimungu kama kuwahudumiwa waja na watu wake,” amesema Profesa Kabudi.
Ametaka wateule hao kuwa waaminifu na wajiepushe kutamani masuala ya kando ya majukumu yao.
“Tutunze viapo vyetu, tutunze uaminifu wetu na tujue kazi yoyote tunayopewa na mheshimiwa Rais ni kazi muhimu ya maana na ya thamani na tusitamani nyengine,” amesema
Profesa Kabudi amesema, “ukipewa wajibu huo ni mkubwa, uheshimu, ufanyie kazi, ridhika nao, sio kwa maana yoyote ile, ukijua daraja na daraja jingine liache na hasa unapopewa kazi na mkuu wa nchi.”
Amesema, kasinya Rais Magufuli ya kutaka kuleta maendeleo inatokana dhamira ya kutekeleza ndoto na mipango ya Mwalimu Nyerere.
Amesema nchi inakwenda kutimiza miaka 60 tangu kuwa huru kwa kishindo cha kufanikisha mambo makubwa ndani ya miaka mitano.
0747259169
0747259169