Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Profesa Kabudi: Ukiteuliwa na Rais Magufuli usitamani kazi nyingine
Habari za Siasa

Profesa Kabudi: Ukiteuliwa na Rais Magufuli usitamani kazi nyingine

Prof. Palamaganda Kabudi, Waziri wa katiba na Sheria
Spread the love

PROFESA Palamaganda Kabudi, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, amewataka watumishi wa umma nchini kuwa waadilifu na uaminifu wakiwa kwenye majukumu yao. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Kabudi amesema hayo leo Jumatatu tarehe 6 Julai 2020  Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma kwenye hafla ya Rais John Pombe Magufuli kuapisha viongozi mbalimbali aliowateua hivi karibuni.

Kabudi amesema vyeo walivyopewa ni dhamana yenye thamani mbele ya Mwenyezi Mungu.

“Sisi sote ambao tumepewa dhamana kubwa ya kuwaongoza Watanzania, tujue hakuna kazi ya thamani kubwa machoni mwa Mwenyezimungu kama kuwahudumiwa waja na watu wake,” amesema Profesa Kabudi.

Ametaka wateule hao kuwa waaminifu na wajiepushe kutamani masuala ya kando ya majukumu yao.

Rais John Magufuli

“Tutunze viapo vyetu, tutunze uaminifu wetu na tujue kazi yoyote tunayopewa na mheshimiwa Rais ni kazi muhimu ya maana na ya thamani na tusitamani nyengine,” amesema

Profesa Kabudi amesema, “ukipewa wajibu huo ni mkubwa, uheshimu, ufanyie kazi, ridhika nao, sio kwa maana yoyote ile, ukijua daraja na daraja jingine liache  na hasa unapopewa kazi na mkuu wa nchi.”

Amesema, kasinya Rais Magufuli ya kutaka kuleta maendeleo inatokana dhamira ya kutekeleza ndoto na mipango ya Mwalimu Nyerere.

Amesema nchi inakwenda kutimiza miaka 60 tangu kuwa huru kwa kishindo cha kufanikisha mambo makubwa ndani ya miaka mitano.

2 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!