Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Solskjaer ampigia chapuo Greenwood England
Michezo

Solskjaer ampigia chapuo Greenwood England

Spread the love

Kocha wa Manchester United, Ole Gunnar Solskjaer amempigia debe kinda wake, Mason Greewood katika kikosi cha timu ya Taifa ya England, kutokana na kiwango alichokionyesha kwa hivi karibuni. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Greenwood ambaye mwenye umri wa miaka 18, hivi karibuni amekuwa na kiwango kizuri kwa kufanikiwa kufunga mabao matatu kwenye michezo dhidi ya Bournemouth na Brighton yote ya Ligi Kuu nchini England.

Kocha huyu amesema kuwa kama mchezaji huyo anaweza kumudu kucheza ndani ya Manchester United basi pia ataweza kucheza kwenye klabu na timu yoyote kwa sababu ana ubora ambao wengine hawana.

“Anaweza kucheza kwenye timu ya wakubwa England au hata chini ya miaka 21, mimi sitajali, najua anafanya vizuri kwetu na jambo kubwa kuwa naye,” alisema kocha huyo.

“Kama ameweza kumudu kucheza Manchester United kwa hiyo anaweza kumudu kucheza timu yoyote na Mason anaubora ambao wengine hawana,” aliongezea Solskjaer.

Greenwood ambaye amelelewa kwenye kituo cha Manchester United mpaka sasa ameshacheza michezo 29 ya Ligi Kuu England, na kufunga jumla ya mabao nane toka alipopandishwa kwenye timu ya wakubwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!