Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi Dar kuwavaa wauza silaha
Habari Mchanganyiko

Polisi Dar kuwavaa wauza silaha

Mapanga yakiwa yanauzwa barabarani
Spread the love

JESHI la Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewataka wafanyabiashara kuacha kuuza silaha kama mapanga, majambia, visu, manati na upinde bila utaratibu wa kisheria, anaandika Pendo Omary.

Simon Sirro, Kamishna wa Polisi leo amewaambia waandishi wa habari kuwa biashara hiyo kwa sasa imeshamiri katika barabara ya Nyerere/Tazara kwenye mataa ya kuongoza magari, Chang’ombe na gerezani hali inayohatari usalama wa watu hususan watumiaji wa barabara hizo.

“Baadhi ya wauzaji wa bidhaa hizo, hutumia fursa hiyo kuwatishia watu wakiwa kwenye magari binafsi na yale ya umma na kuwaibia mali mbalimbali kama simu za mkono, saa, mikoba, pochi na kompyuta mpakato,” amesema Sirro.

Sirro amesema silaha hizo zinatakiwa kuuzwa kwenye maduka yenye leseni na kwamba atakayepatikana akifanya biashara hiyo atachukuliwa hatua kali za kisheria.

“Tarehe 12 Januari mwaka huu, kwenye mataa ya Tazara alikamatwa mtuhumiwa Ngoli Salakani (39), akifanya biashara hiyo. Hatua za kisheria zinachukuliwa dhidi yake,” amesema Sirro.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!