KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humprey Polepole ameitaka mikutano ya majimbo na wilaya ya kura za maoni ya kupata wagombea udiwani, ubunge na uwakilishi ndani ya chama hicho iwe wazi kwa vyombo vya habari kushiriki. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea)
Polepole ametoa wito huo leo Jumatatu tarehe 13 Julai 2020 wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma kuelekea shughuli ya kuwaopata wagombea udiwani, ubunge na uwakilishi ndani ya chama hicho katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020.
Amesema, uwazi aliouonyesha mwenyekiti wa chama hicho, Rais John Pombe Magufuli katika mkutano wa Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM na mkutano mkuu iliyoanza tarehe 10 hadi 11 Julai 2020 jijini Dodoma unapaswa kuigwa katika mikutano ya kura za maoni.
Katika mikutano hiyo, hasa wa NEC ambao kwa mara ya kwanza ulirushwa moja kwa moja na vyombo vya habari ambao pamoja na mambo mengine, ulipiga kura za kumpanga mgombea urais wa Zanzibar na kumpendekeza Rais Magufuli kuwa mgombea urais wa Tanzania.
Vyombo vya habari vilishiriki mwanzo, mwisho ikiwemo uhesabuji wa kura ambapo Dk. Hussein Ali Mwinyi aliibuka mshindi kwa kupata kura 129 sawa na asilimia 78.65, Shamsi Vuai Nahodha kura 16 na Dk. Khalid Salum Muhamed akipata kura 19
Soma zaidi hapa
Ccm yapiga ‘stop’ michango holela za ubunge na udiwani
Polepole amesema, hilo linapaswa kuigwa na mikutano ya kura za maoni kwa wagombea kuruhusiwa wao wenyewe kushiriki kuhesabu kura zao na kama kamati za siasa, zitakuwa na uwezo wa kuarika vyombo vya habari kurusha moja kwa moja wafanye hivyo ili kuendeleza kile alichokiasisi Rais Magufuli.
Shughuli ya uchukuaji na urejeshaji wa fomu za udiwani, ubunge na uwakilishi unaanza kesho Jumanne tarehe 14 hadi 17 Julai 2020.
Soma zaidi hapa
Leave a comment