CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeanza kusambaza picha ya Tundu Lissu kama alivyoahidi Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe mbele ya waandishi wa habari jana Makao Makuu ya chama hicho, anaandika Faki Sosi.
Picha hiyo inayomwonesha Tundu Lissu akiwa amelazwa katika Hospitali Kuu ya Nairobi, Kenya akiwa na tabasamu, huku akipunga mkono, ni ya kwanza tangu kushambuliwa kwa risasi, ikiwa ni siku 41 tangu kutoa kwa tukio hilo.
Pamoja na picha hiyo kutokuwa na maneno lakini, muonekane wake unaonesha kuwa afya yake imeeimarika kama ilivyoelezewa na Mbowe jana.
Mbowe alieleza kuwa watasambaza picha za Lissu, video yake pamoja na sauti itakayoelezea tukio lililompata ikiwa sehemu ya kutoa taarifa kwa umma.
Leave a comment