MWENYEKITI wa Mtandao wa Wanafunzi nchini (TSNP), Abdull Nondo ametiwa mbaroni na jeshi la Polisi usiku kuamkia leo. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).
Akizungumza na MwanaHALISI Online Hellen Sisya Ofisa Habari wa Mtandao huo amethibitisha kushikiliwa kwa kiongozi huyo.
Sisya amesema kuwa Nondo alikamatwa akiwa viunga vya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam usiku wa jana Julai 26 na askari wa chuo hicho.
Paul Kisabo, Mkurugenzi wa Idara ya Sheria wa TSNP, amesema kuwa Nondo amekamatwa akiwa eneo la Mgahawa wa chuo na
askari wa auxiliary.
“Tumefika kituo cha polisi chuo tumekuta Abdul Nondo anachukuliwa maelezo lakini alikataa kuyasaini sababu hakuwa na msaada wa kisheria akiwa anachukuliwa maelezo.
“Sababu ya kukamatwa ni eti amefanya criminal tresspass chuoni, tumeongea na mkuu wa kituo ili tuweze kuondoka na Nondo, imeshindikana kwa sababu za kiusalama,” amesema Kisabo.
Leave a comment