Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Nondo akamatwa tena na Polisi
Habari MchanganyikoTangulizi

Nondo akamatwa tena na Polisi

Abdul Nondo, Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana ACT-Wazalendo
Spread the love

MWENYEKITI wa Mtandao wa Wanafunzi nchini (TSNP), Abdull Nondo ametiwa mbaroni na jeshi la Polisi usiku kuamkia leo. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Akizungumza na MwanaHALISI Online Hellen Sisya Ofisa Habari wa Mtandao huo amethibitisha kushikiliwa kwa kiongozi huyo.

Sisya amesema kuwa Nondo alikamatwa akiwa viunga vya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam usiku wa jana Julai 26 na askari wa chuo hicho.

Paul Kisabo, Mkurugenzi wa Idara ya Sheria wa TSNP, amesema kuwa Nondo amekamatwa akiwa eneo la Mgahawa wa chuo na
askari wa auxiliary.

“Tumefika kituo cha polisi chuo tumekuta Abdul Nondo anachukuliwa maelezo lakini alikataa kuyasaini sababu hakuwa na msaada wa kisheria akiwa anachukuliwa maelezo.

“Sababu ya kukamatwa ni eti amefanya criminal tresspass chuoni, tumeongea na mkuu wa kituo ili tuweze kuondoka na Nondo, imeshindikana kwa sababu za kiusalama,” amesema Kisabo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!