Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Michezo Ngoma aendelea kuitia hasara Azam FC
Michezo

Ngoma aendelea kuitia hasara Azam FC

Spread the love

MSHAMBULIAJI wa Azam FC, Donald Ngoma bado ataendelea kuwa nje ya uwanja baada ya kuendelea kutibu jeraha lake la goti lililomsumbua kwa muda mrefu licha ya kwenda nchini Afrika Kusini kwa matibabu. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Msemaji wa klabu hiyo, Jaffari Maganga amesema kuwa kwa sasa hawawezi kumtumia mshambuliaji huyo bila kupata kibari kutoka kwa daktari wa timu hiyo ambaye anafahamu lini Ngoma anatakiwa kurudi uwanjani kutokana na ratiba aliyompangia.

“Mshambuliaji huyo anasaubiri tarehe yake ili aweze kurudi uwanjani lakini mpaka sasa wanafanya mazoezi ya utimamu wa mwili kwa hiyo hivi karibuni watawapokea na kujiunga na wenzao,” amesema Jaffar.

Ngoma ambaye alisajiliwa akitokea Yanga mwishoni mwa msimu wa 2017/18 lakini mpaka sasa ajafanikiwa kucheza mchezo wowote akiwa na timu hiyo licha ya viongozi wake kusema itamchukua wiki tatu tu kupona jeraha lake hilo la goti lakini mpaka sasa bado hali tete.

Katika hatua nyingine klabu ya hiyo inatarajia kucheza mchezo wake wa kirafiki dhidi ya Arusha United inayoshiriki ligi daraja la kwanza kwa ajili ya kuwapa nafasi wachezaji wao ambao hawakuweza kucheza katika michezo miwili iliyopita ya ligi kutokana na kukosa nafasi katika kikosi cha kwanza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!