Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa NEC yaivimbia Marekani 
Habari za SiasaTangulizi

NEC yaivimbia Marekani 

Mwenyekiti wa NEC, Semistocles Kaijage
Spread the love

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imeitaka Marekani kueleza namna Uchaguzi Mkuu wa Tanzania ulivyoingiliwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumza na gazeti moja la kila siku kuhusu kauli ya Wazir wa Mambo ya Nje ya Marekani, Michael Pompeo kuwawekea vikwazo waliohusika na kuvuruga uchaguzi huo, Jaji Semistocles Kaijage, Mwenyekiti wa NEC amesema ‘hayo ni maoni yao.’

Amesema, si vema kueleza mambo kiujumla jumla na kwamba, wanapaswa kueleza ni kwa namna gani uchaguzi mkuu wa Tanzania ulivurugwa ama kuingiliwa.

Jaji Kaijage amesisitiza, uchaguzi mkuu ulihudhuriwa na waangalizi wa nje na kuwa, kama kungekuwa na tatizo lingejionesha kwenye ripoti zao.

Taarifa ya Marekani kuweka vikwanzo kwa baadhi ya maofisa wa Tanzania bila kutaja majina, iliwekwa hadharani tarehe 19 Januari 2021.

Tamko la Pempoe limelalamikia kuwepo kwa uvunjifu wa haki za binadamu, wapinzani kuenguliwa kwenye kinyang’anyiro, kukamatwa, kunyanyaswa na hata ufungaji wa intaneti.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!