Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Nape  Nnauye ajiuzulu
Habari za SiasaTangulizi

Nape  Nnauye ajiuzulu

Spread the love

NAPE Nnauye, amejiuzulu uenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maliasili na Utalii. Kujiuzulu kwake, kunatokana kile kinachoitwa, “kugoma kunyofoa baadhi ya taarifa kwenye ripiti ya kamati yake.” Anaripoti Mwandishi Wetu kutoka Dodoma … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya Kamati ya Bunge ya Maliasili na Utalii zinasema, Nape amejiuzulu baada ya kushinikizwa na baadhi ya wakubwa ndani ya chama chake.

“Ni kweli kwamba Nape amejiuzulu. Ni baada ya kutaka ripoti ya Kamati ya Bunge ya Maliasili na Utalii, iliombe Bunge kuundwa kwa Kamati Teule, ili kuchunguza utaratibu uliotumika wa kufuta mashamba ya baadhi ya wananchi,” ameeleza mjumbe mmoja wa kamati hiyo.

Ameongeza, “lakini serikali haitaki kuundwa kwa Kamati hiyo. Hivyo imeamua kutumia Kamati ya wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kumlazimisha kujiuzulu.”

Taarifa zinasema, tayari Nape amemuandikia barua Spika ya kumjulisha kujiuzulu. Katibu wa Bunge, Steven Kigaigai, amemthibitishia mwandishi wa habari hii kujiuzulu kwa mwanasiasa huyo.

Machi mwaka juzi, Nape aling’olewa kwenye nafasi ya uwaziri wa habari, utamaduni, Sanaa na michezo.

Mbunge huyo wa Mtama mkoani Lindi, alivuliwa wazifa wake huo, siku moja baada ya kupokea ripoti ya Kamati ya uchunguzi wa tukio la uvamizi wa kituo cha televisheni cha Clouds. Kituo hicho kilivamiwa na watu wenye silaha, wakiwa na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.

Nape aliwahi kuwa Katibu wa Idara ya Uenezi ya CCM.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

error: Content is protected !!