Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Naibu Spika Tulia apeta Mbeya, Dk. Kimei chali Vunjo
Habari za Siasa

Naibu Spika Tulia apeta Mbeya, Dk. Kimei chali Vunjo

Dk. Tulia Ackson
Spread the love

NAIBU Spika wa Bunge la Tanzania, Dk. Tulia Ackson ameongoza katika kura za maoni Jimbo la Mbeya Mjini kwa tiketi ya CCM kwa kura 843 kati ya kura zote 885 sawana asilimia 95. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mbeya … (endelea)

Mshindi wa pili ni Mahenge Mabula aliyepata kura 16 na mshindi wa tatu akiwa ni Charles Mwakipesile aliyepata kura 11.

Iwapo, Dk. Tulia akipitishwa na chama hicho kugombea, ataumana na wagombea wa vyama vingine akiwemo Joseph Mbilinyi maarufu Sugu wa Chadema.

Katika hatua nyingine, Mkurugenzi Mkuu wa zamani wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei ameangukia pua Jimbo la Vunjo kwa kupata kura 178 akishika nafasi ya pili na aliyeongoza ni Enock Koola aliyepata kura 187 kati ya 567 zilizopigwa na wajumbe.

Charles Kimei

Nafasi ya tatu imeshikwa na Chrispine Meela aliyepata kura 47, wagombea katika kinyang’anyiro hicho walikuwa 35.

Jimbo la Ismani Mkoa wa Iringa, Waziri wa ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi, Willium Lukuvi ameongoza kura za maoni kwa kupata kura 453 kati ya 487.

William Lukuvi (wa kwanza kulia)

Wagombea walikuwa tisa ambapo aliyemfuatia amepata kura 16.

Naye mbunge anayemaliza muda wake wa Mufundi Mjini, Cosato Chumi ameongoza kura za maoni kwa kupata kura 135 akifiatiwa na Bazir Tweve kura 122. 

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online na MwanaHALISI TV kwa habari zaidi

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!