Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwili wa Dk. Mengi kuwasili Jumatatu, kuzikwa Alhamisi
Habari MchanganyikoTangulizi

Mwili wa Dk. Mengi kuwasili Jumatatu, kuzikwa Alhamisi

Michael Ngalo, Mwanasheria wa Familia ya Dk. Reginald Mengi, akizungumza na waandishi wa habari nyumbani kwa marehemu Kinondoni, Dar es Salaam
Spread the love

MWILI wa aliyekuwa Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni za IPP, Dk. Reginald Mengi, unatarajiwa kuwasili nchini Jumatatu wiki ijayo, kutoka Dubai,  Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE). Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Mwanasheria wa Familia ya Marehemu Dk. Mengi, Michael Ngalo ametoa kauli hiyo nyumbani kwa marehemu leo tarehe 3 Mei 2019 wakati akitoa ratiba ya shughuli za mazishi ya Dk. Mengi ambaye alikuwa mfanyabiashara mkubwa nchini.

Wakili Ngalo amesema, Dk. Mengi aliyefariki dunia usiku wa kuamkia tarehe 2 Mei 2019, ataagwa siku ya Jumanne tarehe 7 Mei 2019 kwenye viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.

Na kwamba, baada ya mwili wa Dk. Mengi kuagwa, siku ya Jumatano tarehe 8 Mei 2019 utasafirishwa kuelekea Machame wilayani Moshi, Kilimanjaro.

Akitangaza ratiba hiyo nyumbani kwake Kinondoni leo, Wakili Ngalo amesema, ibada ya mazishi itafanyika siku ya Alhamisi katika Kanisa la KKKT, Kisereni na kisha kuzikwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!