Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Wanaume mnaonyanyaswa jitokezeni – Serikali
Habari Mchanganyiko

Wanaume mnaonyanyaswa jitokezeni – Serikali

Dk. Faustin Ndungulile
Spread the love

SERIKALI imewataka wanaume wanaonyanyaswa kijinsia na wake zao, kutoa taarifa kwenye madawati ya kijinsia. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 3 Mei 2019 na Faustine Ndugulile, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto wakati akijibu swali la nyongeza la Rita Kabati, Mbunge wa Viti Maalum (CCM).

Katika swali lake Rita Kabati ametaka kujua, serikali itatunga lini sheria ya kuwatetea wanaume wanaonyanyaswa kijinsia na wake zao?

Ndugulile amesema, yapo madawati yanayoshughulikia maswala ya unyanyasaji katika vituo vya polisi na maeneo mbalimbali.

Na kwamba, tatizo kubwa ni wanaume kutojitokeza kulalamikia vitendo hivyo badala yake hukaa kimya.

Akijibu swali la msingi la Mbunge wa Vitimaalum, Amina Makilagi (CCM), Ndungulile amesema, serikali inatambua ukatili wa kijinsia ni pamoja na vitendo vya kuwanyanyasa, kuwadhalilisha na kuwadhulumu wanawake na watoto.

Amsema, ukatili wa kingono na kisaikolojia ni sehemu ya ukatili wa kijinsia hivyo ni muhimu kutolewa taarifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi Nyamkumbu wanolewa na GGML kuhusu taaluma ya madini

Spread the loveZAIDI ya Wanafunzi 50 kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana...

Habari Mchanganyiko

Somo la dini: Waislamu waishukia Serikali, wizara yatoa kauli

Spread the loveJUMUIYA na Taasisi za Kiislamu Tanzania, imetupia lawama Serikali ikidai...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!