MWANASHERIA Mkuu wa kwanza Tanzania, Mark Bomani amefariki dunia usiku wa kumakia leo tarehe 11 Septemba 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).
Taarifa zilizopatikana mpaka sasa kutoka kwa wanafamilia wa mwanasheria huyo zinasema, Bomani (76) amefariki dunia alipokuwa akipata matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhmbili (MNH), jijini Dar es Salaam, hata hivyo haijaelezwa maradhi yaliyokuwa yakimsumbua.
Bomani aliongoza Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuanzia mwaka 1965 hadi 1976 chini ya serikali ya kwanza ya Hayati Mwalimu Julius Nyerere.
Leave a comment