Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mpina awatimua wakaguzi mifugo Kituo cha Kibaha
Habari Mchanganyiko

Mpina awatimua wakaguzi mifugo Kituo cha Kibaha

Luhaga Mpina, Waziri wa Mifugo na Uvuvi
Spread the love

WATUMISHI katika Kituo cha Ukaguzi Kibaha mkoa wa Pwani, wameondolewa kazini na serikali kutokana na kushindwa kusimamia rasilimali za sekta ya mifugo na uvuvi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Agizo hilo limetolewa leo tarehe 5 Desemba 2018 na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina katika kikao cha tathmini ya Operesheni Nzagamba awamu ya pili kilichofanyika jijini Dodoma.

Mpina amesema watumishi wasio waadilifu na kushindwa kutekeleza majukumu yao hawana nafasi katika Wizara yake, ndiyo maana ameagiza kuondolewa mara moja kwa watumishi wanaofanya kazi ya ukaguzi wa rasilimali hizo katika kituo cha Kibaha.

Kuhusu operesheni Nzagamba awamu ya pili iliyotekelezwa kipindi cha mwezi Oktoba na Novemba, Mpina amesema operesheni hiyo imedhihirisha kuwa, usimamizi thabiti wa sheria, kanuni na taratibu katika sekta ya mifugo, unaweza kuleta tija kwa kuongeza uzalishaji bora wa mazao ya mifugo ambayo ni malighafi ya viwanda.

Katika hatua nyingine, Mpina alizitaka mamlaka zinazotoa Leseni kwa wafanyabishara wanaosafirisha mifugo nje ya nchi kuweka utaratibu rafiki utakaosaidia kundi hilo kutoa mchango wake katika ujenzi wa Taifa na kuondoa au kupunguza vitendo vya biashara ya magendo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!