Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mpina awatimua wakaguzi mifugo Kituo cha Kibaha
Habari Mchanganyiko

Mpina awatimua wakaguzi mifugo Kituo cha Kibaha

Luhaga Mpina, Waziri wa Mifugo na Uvuvi
Spread the love

WATUMISHI katika Kituo cha Ukaguzi Kibaha mkoa wa Pwani, wameondolewa kazini na serikali kutokana na kushindwa kusimamia rasilimali za sekta ya mifugo na uvuvi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Agizo hilo limetolewa leo tarehe 5 Desemba 2018 na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina katika kikao cha tathmini ya Operesheni Nzagamba awamu ya pili kilichofanyika jijini Dodoma.

Mpina amesema watumishi wasio waadilifu na kushindwa kutekeleza majukumu yao hawana nafasi katika Wizara yake, ndiyo maana ameagiza kuondolewa mara moja kwa watumishi wanaofanya kazi ya ukaguzi wa rasilimali hizo katika kituo cha Kibaha.

Kuhusu operesheni Nzagamba awamu ya pili iliyotekelezwa kipindi cha mwezi Oktoba na Novemba, Mpina amesema operesheni hiyo imedhihirisha kuwa, usimamizi thabiti wa sheria, kanuni na taratibu katika sekta ya mifugo, unaweza kuleta tija kwa kuongeza uzalishaji bora wa mazao ya mifugo ambayo ni malighafi ya viwanda.

Katika hatua nyingine, Mpina alizitaka mamlaka zinazotoa Leseni kwa wafanyabishara wanaosafirisha mifugo nje ya nchi kuweka utaratibu rafiki utakaosaidia kundi hilo kutoa mchango wake katika ujenzi wa Taifa na kuondoa au kupunguza vitendo vya biashara ya magendo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!