Friday , 2 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Mpina awatimua wakaguzi mifugo Kituo cha Kibaha
Habari Mchanganyiko

Mpina awatimua wakaguzi mifugo Kituo cha Kibaha

Luhaga Mpina, Waziri wa Mifugo na Uvuvi
Spread the love

WATUMISHI katika Kituo cha Ukaguzi Kibaha mkoa wa Pwani, wameondolewa kazini na serikali kutokana na kushindwa kusimamia rasilimali za sekta ya mifugo na uvuvi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Agizo hilo limetolewa leo tarehe 5 Desemba 2018 na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina katika kikao cha tathmini ya Operesheni Nzagamba awamu ya pili kilichofanyika jijini Dodoma.

Mpina amesema watumishi wasio waadilifu na kushindwa kutekeleza majukumu yao hawana nafasi katika Wizara yake, ndiyo maana ameagiza kuondolewa mara moja kwa watumishi wanaofanya kazi ya ukaguzi wa rasilimali hizo katika kituo cha Kibaha.

Kuhusu operesheni Nzagamba awamu ya pili iliyotekelezwa kipindi cha mwezi Oktoba na Novemba, Mpina amesema operesheni hiyo imedhihirisha kuwa, usimamizi thabiti wa sheria, kanuni na taratibu katika sekta ya mifugo, unaweza kuleta tija kwa kuongeza uzalishaji bora wa mazao ya mifugo ambayo ni malighafi ya viwanda.

Katika hatua nyingine, Mpina alizitaka mamlaka zinazotoa Leseni kwa wafanyabishara wanaosafirisha mifugo nje ya nchi kuweka utaratibu rafiki utakaosaidia kundi hilo kutoa mchango wake katika ujenzi wa Taifa na kuondoa au kupunguza vitendo vya biashara ya magendo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari Mchanganyiko

Serikali yakabidhi eneo la mahakama ya Afrika ya haki za binadamu

Spread the loveSerikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa...

Habari Mchanganyiko

Udhamini wa NMB mikutano ya ALAT wafikia 1.2 bilioni

Spread the loveBENKI ya NMB imeendelea kufanya kazi kwa karibu na Asasi...

Habari Mchanganyiko

Dk. Gwajima atoa maelekezo kwa maofisa maendeleo nchini

Spread the love  WAZIRI wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Watoto,...

error: Content is protected !!