Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mch. Msigwa: Nakubalika
Habari za Siasa

Mch. Msigwa: Nakubalika

Mch. Peter Msigwa
Spread the love

MCHUNGAJI Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini, amesema kila baada ya miezi mitatu, hufanya utafiti kubaini idadi ya wananchi wanaomuunga mkono jimboni humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Mchungaji Msigwa ametoa kauli hiyo alipokuwa kwenye mahojiano na Kituo cha Redio cha East Africa.

Amesema, matokeo ya utafiti anaoufanya yamebaini kwamba kati ya wananchi 10 jimboni humo, saba wanamuunga mkono, wawili wanaunga mkono Chama cha Mapinduzi (CCM), na mmoja hana uamuzi juu ya suala hilo.

Mchungaji Msigwa amesema kufuatia matokeo ya utafiti huo, atagombea tena katika jimbo hilo, kwenye Uchaguzi Mkuu wa Mwezi Oktoba 2020.

“Nagombea,  wananchi wananihitaji bado. Nimekwua na tabia ya kufanya utafiti kila baada ya miezi mitatu . Katika utafiti niliofanya kati ya watu kumi, saba wananiunga mkono, wawili wanaiunga mkono CCM na mmoja hana uamuzi,” amesema Msigwa .

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!