Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge upinzani akimbilia CCM
Habari za Siasa

Mbunge upinzani akimbilia CCM

Spread the love

REHEMA Migira, Mbunge wa Viti Maalum kupitia Chama cha Wananchi (CUF), amekimbilia Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Mwandishi Wetu, Tabora…(endelea).

Akitangaza kwenye sherehe ndogo iliyofanywa na chama hicho Tabora leo tarehe 15 Juni 2020, Rehema amesema, amejiunga na chama hicho baada ya kuridhishwa na utendaji kazi wa Rais John Magufuli ambaye pia ni mwenyekiti wa CCM Taifa.

“Nikiwa na akili zangu timamu na kwa utashi wangu mimi mwenyewe, nimeamua kwa ridhaa yangu mimi mwenyewe bila kushikiwa mtutu wa bunduki kurudi chama cha mapinduzi,” amesema huku akipigiwa vigelegele na kuongeza:

“…maamuzi haya sikuyafanya eti kwa sababu napenda rangi za kijani, kuna sababu ambazo zimepelekea mimi leo niamue kurudi chama cha mapinduzi, CCM imekuwa ni ya wazalendo.”

Amesema, sera za CCM zinatekelezwa kupitia Rais Magufuli kwa kushirikiana na wasaidizi wake. “Vitendo hivyo vimesababisa hata sisi wapinzani tushawishike,” amesema.

1 Comment

  • Mtoa post rekebisha lugha, hakuna anae hamia ccm, bali wanarudi ccm, maana walitoka humo humo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!