Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mbunge ataka wanaume wasiofanyiwa tohara wasioe
Habari Mchanganyiko

Mbunge ataka wanaume wasiofanyiwa tohara wasioe

Spread the love

RUKIA Kassim Ahmed, Mbunge Viti Maalumu kupitia Chama cha Wananchi (CUF), ameitaka Serikali ya Tanzania kuwazuia wanaume wasiotahiriwa kuoa, ili kuwakinga wanawake dhidi ya ugonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Rukia ametoa hoja hiyo leo Jumanne tarehe 9 Juni 2020, wakati akiuliza swali kuhusu mkakati wa serikali katika kuweka zuio la kuoa kwa wanaume ambao hawajatahiriwa.

“Imethibitika kuwa saratani ya mlango wa kizazi inasababishwa na virusi vinavyopatikana kwa wanaume ambao hawajatahiriwa. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuweka zuio la kuoa kwa wanaume ambao hawajatahiriwa,” ameuliza swali hilo kwa njia ya mtandao wa Bunge.

Akijibu swali hilo kwa njia hiyohiyo, Waziri wa Afya amesema, Serikali haina mkakati wa kuweka zuio hilo, bali imeweka mikakati dhidi ya kujikinga na Kirusi cha Human Papiloma, kinachosababishwa saratani hiyo, kwa njia ya kujamiiana.

“Serikali imeweka mikakati dhidi ya kujikinga na kirusi hiki ikiwemo utoaji wa chanjo dhidi ya kirusi cha papilloma kwa wasichana wa umri ya miaka 9-14 kote nchini, “ amesema Waziri wa Afya.

Sambamba na chanjo hiyo, Waziri wa Afya amesema, Serikali inaendelea kuhamasisha wanaume kufanya tohara, kwa kuwa wanaume hao wako kwenye hatari ya kuwa na kirusi hicho, kinachosababisha saratani.

“Tunahakikisha tunatoa elimu juu ya kubadilisha tabia, ikiwepo pia kuhamasisha kufanya tohara kwa wanaume, kwani wanaume waliofanyiwa tohara hawapo kwenye hatari ya kuwa na kirusi hiki (cha Papiloma) kinachosababisha saratani,” amesema Waziri wa Afya.

Waziri huyo amesema, “kwa wale wanawake ambao wameshapata maambukizo ya kirusi cha papilloma, tunahamasisha kufanya uchunguzi wa kutambua uwepo wa mabadiliko ya awali ya saratani ya mlango wa kizazi na kuwapatia tiba ya ugandishaji kwa kutumia kimiminika cha gesi ya carbondioxide.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!