Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Mbunge ataka wanaume wasiofanyiwa tohara wasioe
Habari Mchanganyiko

Mbunge ataka wanaume wasiofanyiwa tohara wasioe

Spread the love

RUKIA Kassim Ahmed, Mbunge Viti Maalumu kupitia Chama cha Wananchi (CUF), ameitaka Serikali ya Tanzania kuwazuia wanaume wasiotahiriwa kuoa, ili kuwakinga wanawake dhidi ya ugonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Rukia ametoa hoja hiyo leo Jumanne tarehe 9 Juni 2020, wakati akiuliza swali kuhusu mkakati wa serikali katika kuweka zuio la kuoa kwa wanaume ambao hawajatahiriwa.

“Imethibitika kuwa saratani ya mlango wa kizazi inasababishwa na virusi vinavyopatikana kwa wanaume ambao hawajatahiriwa. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuweka zuio la kuoa kwa wanaume ambao hawajatahiriwa,” ameuliza swali hilo kwa njia ya mtandao wa Bunge.

Akijibu swali hilo kwa njia hiyohiyo, Waziri wa Afya amesema, Serikali haina mkakati wa kuweka zuio hilo, bali imeweka mikakati dhidi ya kujikinga na Kirusi cha Human Papiloma, kinachosababishwa saratani hiyo, kwa njia ya kujamiiana.

“Serikali imeweka mikakati dhidi ya kujikinga na kirusi hiki ikiwemo utoaji wa chanjo dhidi ya kirusi cha papilloma kwa wasichana wa umri ya miaka 9-14 kote nchini, “ amesema Waziri wa Afya.

Sambamba na chanjo hiyo, Waziri wa Afya amesema, Serikali inaendelea kuhamasisha wanaume kufanya tohara, kwa kuwa wanaume hao wako kwenye hatari ya kuwa na kirusi hicho, kinachosababisha saratani.

“Tunahakikisha tunatoa elimu juu ya kubadilisha tabia, ikiwepo pia kuhamasisha kufanya tohara kwa wanaume, kwani wanaume waliofanyiwa tohara hawapo kwenye hatari ya kuwa na kirusi hiki (cha Papiloma) kinachosababisha saratani,” amesema Waziri wa Afya.

Waziri huyo amesema, “kwa wale wanawake ambao wameshapata maambukizo ya kirusi cha papilloma, tunahamasisha kufanya uchunguzi wa kutambua uwepo wa mabadiliko ya awali ya saratani ya mlango wa kizazi na kuwapatia tiba ya ugandishaji kwa kutumia kimiminika cha gesi ya carbondioxide.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!