Tuesday , 5 December 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Maelfu waaga mwili wa Floyd
Kimataifa

Maelfu waaga mwili wa Floyd

Spread the love

MAELFU ya Wamarekani, wamejitokeza katika Kanisa la Houston kuuaga mwili wa George Floyd, mmarekani mweusi aliyeuawa na polisi wa Minnesota na kusababisha kuibuka kwa maandamano ndani na nje ya taifa hilo. Inaripoti mitandao ya kimataifa…(endelea).

Waombolezaji hao waliovaa fulana zenye picha ya Floyd, wametoa heshima zao za mwisho leo tarehe 9 Juni 2020, kabla ya mwili huo kuzikwa jijini humo. Watu zaidi ya 6,000 wanatajwa kuhudhuria mazishi hao.

Kifo cha Floyd kimechukuliwa kwa uzito wa pekee baada ya Wamarekani kuchoshwa na mauaji ya watu weusi, vifo vingine vinavyotajwa kabla ya Floyd ni cha Eric Garner, Michael Brown, Ahmaud Arbery na Trayvon Martin.

Kwenye salamu hizo za mwisho, Philonise Floyd ambaye ni kaka wa Floyd amesema “inaumiza sana,” kushiriki mashizi yaliyosababishwa na walinda usalama wa raia na mali zao.

Jeneza la Floyd limesindikizwa na polisi wa Houston mpaka kanisani ambapo taratibu zote zimesimamiwa na polisi hao, kwa utaratibu unaokubwalika.

Awali, akizungumza na wakazi wa Texas, Philonise amesema kinachofanyika Marekani kwa sasa ni kikubwa kuliko mdogo wake George kwa kuwa, kinakwenda kubadilisha kila kitu.

“Hiki kinachofanyika ni kikubwa kuliko George kwa sasa. Tumefanikiwa kuzuia hofu za raia kwa polisi,” amesema Philonise.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Muandamanaji ajichoma moto akipinga vita Palestina, Israel

Spread the loveMUANDAMANAJI moja ambaye hajafahamika jina, yuko mahututi hospitalini akitetea uhai...

Kimataifa

Urusi kuongeza wanajeshi ikijihami dhidi ya NATO

Spread the loveSERIKALI ya Urusi iko katika mpango wa kuongeza wanajeshi wake,...

Kimataifa

Israel yarejesha mashambulizi Gaza ikilaumu Hamas kukiuka makubaliano

Spread the loveJESHI la Israel, limerejesha mashambulizi katika ukanda wa Gaza, baada...

Kimataifa

Papa Francis kumfukuza Kardinali anayepinga mageuzi Kanisa Katoliki

Spread the loveKIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, anadaiwa kupanga kumfumkuza...

error: Content is protected !!