Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe atinga mahakamani kwa Sugu
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe atinga mahakamani kwa Sugu

Freeman Mbowe akiwasili mahakamani kusikiliza kesi ya Sugu
Spread the love

MWENYEKITI WA CHADEMA, Freeman Mbowe amewasili katika Mahakama ya Mkoa wa Mbeya, kuhudhuria kesi inayomkabili Mbunge wa Mbeya, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ na Katiku Mkuu wa Kanda ya Nyasa, Emmanuel Masonga, inayoendelea mahakamani hapo. Anaripoti Mwandishi Wetu.

Sugu na Masonga wameshtakiwa kwa kosa la kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli ambayo waliyatoa katika mkutano wa hadhara walioufanya Desemba 30 mwaka jana wakiwa viwanja vya Shule ya Msingi Mwenge jijini Mbeya.

Mbowe alihudhuria mahakamani leo Jumatano Januari 24, 2018 kwa ajili ya kusikiliza kesi ya uchochezi inayomkabili Mbunge huyo na mwenzake kwa lengo la kuwatia nguvu na kuhakikisha haki inatendeka kwa watuhumiwa hao.

Mwenyekiti Mbowe ambaye ameongozana na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mbeya, Sophia Mwakagenda ameingia majira ya saa 3.30 asubuhi hii katika viunga vya mahakama kwa ajili ya kusikiliza kesi hiyo na tayari ameingia kwenye chumba cha mahakama.

Sugu pamoja na Masonga walifikishwa mahakamani hapo kwa mara kwanza Januari 19, 2018 lakini  mahakama ilizuia dhamana zao na kuwarejesha rumande hadi.

Siku hiyo hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama hiyo, Michael Mteite alitoa uamuzi wa kuwarejesha rumande, kwamba kesi hiyo inatakiwa isikilizwe mfululizo kwa muda mfupi na washtakiwa wakiwa wanafika mahakamani hapo wakitokea mahabusu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!