Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe atinga mahakamani kwa Sugu
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe atinga mahakamani kwa Sugu

Freeman Mbowe akiwasili mahakamani kusikiliza kesi ya Sugu
Spread the love

MWENYEKITI WA CHADEMA, Freeman Mbowe amewasili katika Mahakama ya Mkoa wa Mbeya, kuhudhuria kesi inayomkabili Mbunge wa Mbeya, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ na Katiku Mkuu wa Kanda ya Nyasa, Emmanuel Masonga, inayoendelea mahakamani hapo. Anaripoti Mwandishi Wetu.

Sugu na Masonga wameshtakiwa kwa kosa la kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli ambayo waliyatoa katika mkutano wa hadhara walioufanya Desemba 30 mwaka jana wakiwa viwanja vya Shule ya Msingi Mwenge jijini Mbeya.

Mbowe alihudhuria mahakamani leo Jumatano Januari 24, 2018 kwa ajili ya kusikiliza kesi ya uchochezi inayomkabili Mbunge huyo na mwenzake kwa lengo la kuwatia nguvu na kuhakikisha haki inatendeka kwa watuhumiwa hao.

Mwenyekiti Mbowe ambaye ameongozana na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mbeya, Sophia Mwakagenda ameingia majira ya saa 3.30 asubuhi hii katika viunga vya mahakama kwa ajili ya kusikiliza kesi hiyo na tayari ameingia kwenye chumba cha mahakama.

Sugu pamoja na Masonga walifikishwa mahakamani hapo kwa mara kwanza Januari 19, 2018 lakini  mahakama ilizuia dhamana zao na kuwarejesha rumande hadi.

Siku hiyo hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama hiyo, Michael Mteite alitoa uamuzi wa kuwarejesha rumande, kwamba kesi hiyo inatakiwa isikilizwe mfululizo kwa muda mfupi na washtakiwa wakiwa wanafika mahakamani hapo wakitokea mahabusu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!