Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe apata ulinzi wa Polisi
Habari za Siasa

Mbowe apata ulinzi wa Polisi

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

JESHI la Polisi wilayani Hai mkoa wa Kilimanjaro, limevamia mkutano wa ndani wa Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa, kwa kile kilichoelezwa kuwa ni, kumlinda kiongozi huyo na wafuasi wake. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Tukio hilo limetokea leo tarehe 30 Septemba 2019 baada ya Lengai Ole Sabaya, Mkuu wa Wilaya ya Hai kuagiza polisi kufika katika mkutano huo, kwa ajili ya kufuatilia agenda zake.

Ole Sabaya ameeleza kuwa, amechukua hatua hiyo kwa ajili ya kumlinda Mbowe, viongozi na wafuasi wa Chadema waliohudhuria katika mkutano huo, uliofanyika katika ofisi za Chadema za Wilaya ya Hai.

Mkuu huyo wa wilaya amesema, wanaoshiriki katika mkutano huo, hawana sababu ya kutaharuki kama wamefanya mkutano huo kwa nia njema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!